JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA


Kumb. Na EA.7/96/01/I/39                                                                             10 Mei, 2016


TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni chombo ambacho kimeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu 29(1). Kwa mujibu wa Sheria hiyo, chombo hiki, pamoja na kazi zingine kimepewa jukumu la kutangaza nafasi wazi za kazi zinazotokea katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Waajiri (Taasisi za Umma).

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi ya Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 188 kwa ajili ya Wizara, Taasisi zinazojitegemea na mamlaka za Serikali za Mitaa kama inavyoonyesha hapa chini.

NB: MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.        
i.     Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45
ii.   Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa. iii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
iv.      Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
v.        Maombi   yote   yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. 
-      Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates. - Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI 
-      Computer Certificate 
-      Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
-      Picha moja “Passport size” ya hivi karibuni.
vi.      Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
vii.     Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA). viii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
ix.      Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
x.        Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
xi.      Mwisho wamaombi ni tarehe 24 Mei, 2016. xii. Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya ajira HAURUHUSIWI.
             
xiii.      Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa
Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo; http://portal.ajira.go.tz/
(Anuani hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Sektretarieti ya ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa Recruitment Portal’)

xiv.      MUHIMU: KUMBUKA KUWEKA (ATTACH) BARUA YAKO YA MAOMBI. ANUANI YA BARUA HIYO IELEKEZWE KWA KATIBU, OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA S.L.P 63100 DAR ES SALAAM.



1.0     AFISA UFUGAJI NYUKI DARAJA LA II (BEEKEEPING OFFICER  II) – NAFASI- 5(LINARUDIWA)
1.1     MAJUKUMU YA KAZI
      Kusimamia uanzishaji wa hifadhi za nyuki na manzuki.
      Kutangaza Sera na Sheria za ufugaji nyuki.
      Kufundisha masomo ya fani ya ufugaji nyuki.
      Kukusanya takwimu za rasilimali na ufugaji nyuki. Kupanga na kupima ubora wa mazao ya nyuki.

1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Shahada katika fani ya Ufugaji Nyuki au Sayansi ya Elimu ya Mimea, Elimu ya Wadudu au Elimu ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

1.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.D kwa mwezi

2.0 DEREVA DARAJA LA II (DRIVER II) – NAFASI 31
2.1 MAJUKUMU YA KAZI (LINARUDIWA)
      Kuendesha magari ya abiria, magari madogo na malori
      Kuhakikisha gari na vyombo vyake vipo katika hali nzuri wakati wote, na kufanya uchunguzi wa gari kabla na baada ya safari ili kugundua ubovu unaohitaji matengenezo,
      Kufanya matengenezo madogo madogo katika gari,
      Kutunza na kuandika daftari la safari “Log-book” kwa safari zote.

2.2 SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa wenye Cheti cha Mtihani wa Kidato cha IV, Wenye Leseni daraja la “C” ya uendeshaji pamoja na uzoefu wa kuendesha magari kwa muda usiopungua miaka mitatu bila kusababisha ajali na wenye Cheti cha Majaribio ya ufundi Daraja la II (Trade test II).

2.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali ngazi ya Mshahara TGOS. Akwa mwezi.

3.0 MPISHI DARAJA LA II (COOK II ) NAFASI – 7(LINARUDIWA)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee  na Watoto. Wapishi hawa watafanya kazi ya kuwapikia wanachuo katika vyuo vya maendeleo ya wananchi
3.1 MAJUKUMU YA KAZI
      Kuandaa chakula cha wanachuo kulingana na Menyu na idadi ya wanachuo
      Kupika chakula cha wanachuo
      Kutoa ushauri kwa uongozi wa chuo kuhusu chakula cha wanachuo.
      Kusimamia jiko.
3.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya cheti yasiyopungua mwaka mmoja katika moja ya fani ya “food Production” yatolewayo na vyuo vya Forodhani (Dar es Salaam),Masoka (Moshi), Arusha Hotel, Y.M.C.A (Moshi), VETA (mikumi) na Vision Hotel (Dar es Salaam) kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali. 
3.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGSCkwa mwezi.

4.0     MLINZI - NAFASI-  15(LINARUDIWA)
4.1     MAJUKUMU YA KAZI
  Kuhakikisha kwamba mali yoyote ya ofisi inayotolewa langoni (nje ya ofisi) ina hati ya idhini.
  Kuhahikisha kuwa mali yote inayoingizwa langoni inazo hati za uhalali wake.
  Kulinda usalama wa majengo, ofisi na mali za ofisi mchana na usiku.
  Kuhakikisha kwamba milango na madirisha yote yamefungwa ipasavyo mwisho wa saa za kazi.
  Kuhakikisha kwamba wageni wote wanaoingia katika eneo la ofisi wana idhini ya kufanya hivyo.
  Kupambana na majanga yoyote yatakayotokea katika sehemu ya kazi kama vile, moto, mafuriko n.k na kutoa taarifa katika vyombo vinavyohusika kama vile, moto, mafuriko n.k na kutoa taarifa katika vyombo vinavyohusika.
  Kutoa ushauri wa jinsi ya kuboresha huduma ya ulinzi mahali pa kazi.

4.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha Nne waliofuzu mafunzo ya mgambo/polisi/JKT au Mafunzo ya Zimamoto kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali.

4.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGOS.A 

5.0     AFISA MISITU DARAJA LA II (FORESTRY OFFICER GRADE II) –NAFASI- 4(LINARUDIWA)
5.1     MAJUKUMU YA KAZI
  Kusimamia upandaji na uhudumiaji wa miti na misitu.
  Kusimamia uendelezaji wa misitu ya kupandwa isiyozidi hekta 5,000 au ya asili isiyozidi hekta 10,000.
  Kufanya utafiti wa misitu.
  Kutekeleza Sera na Sheria za misitu.
  Kuendesha mafunzo ya Wasaidizi Misitu.
  Kukusanya takwimu za misitu.
  Kufanya ukaguzi wa misitu.
  Kupanga na kupima madaraja ya mbao.
  Kudhibiti leseni na uvunaji wa miti.
  Kutoa ushauri na mafunzo kwa wananchi juu ya uendelezaji na matumizi endelevu ya miti kwa wananchi.
  Kufanya ukadiriaji wa rasilimali za misitu.
  Kupima maeneo na kuchora ramani za misitu.

5.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Shahada ya Misitu kutoka chuo Kikuu cha kilimo cha Sokoine au Vyuo Vikuu vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

5.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.D kwa mwezi.
6.0     MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA II – NAFASI- 5(LINARUDIWA)
6.1     MAJUKUMU YA KAZI
  Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi na mbuga za wanyamapori.
  Kusimamia utekelezaji wa taratibu za uwindaji na utalii.
  Kutekeleza kazi za maendeleo katika Mapori ya Akiba.
  Kuhakiki ulinzi wa nyara za Serikali.
  Kuhakiki vifaa vya doria.
  Kudhibiti usafirishaji wa wanyamapori na nyara nje na ndani ya nchi.
  Kudhibiti matumizi ya magari ya doria.
  Kuratibu uingiaji wa wageni katika Mapori ya Akiba.
  Kusimamia uwindaji wa kitalii.
  Kudhibiti na kusimamia umilikaji wa nyara.
  Kuweka mikakati ya kudhibiti moto mkali.
  Kukusanya takwimu za wanyamapori na mimea.

6.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au Kidato cha VI, wenye stashahada ya Uhifadhi wa Wanyamapori Mweka au chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

6.3    MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B na C kwa mwezi.

7.0     MFUGAJI NYUKI MSAIDIZI DARAJI LA II – NAFASI – 5(LINARUDIWA)
7.1     MAJUKUMU YA KAZI
  Kusimamia manzuki.
  Kutunza hifadhi za nyuki.
  Kukusanya takwimu za ufugaji nyuki.
  Kutunza kumbukumbu za kazi za utafiti.
  Kuondoa nyuki wanaodhuru binadamu na mifugo.
  Kutoa leseni za biashara ya mazao ya nyuki.
  Kutoa ushauri wa kitaalam kwa wananchi juu ya ufugaji endelevu wa nyuki na matumizi bora ya mazao ya nyuki.
  Kutunza makundi ya nyuki wanaouma na wasiouma.

7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne au Sita wenye Astashahada (Cheti) au
Stashahada (Diploma) ya Ufugaji Nyuki kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

7.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B na TGS kwa mwezi.

8.0     DOBI DARAJA LA II – NAFASI 1 (LINARUDIWA)
8.1     MAJUKUMU YA KAZI
Kufanya uchambuzi wa nguo kwa ajili ya kuosha, kukausha, kunyoosha na kuzifungasha.

8.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne waliofuzu mafunzo ya miaka miwili au mitatu     katika fani     ya        Dobi    (Laundry        Services)       kutoka            katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.


8.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGOS. C kwa mwezi.

9.0     MTUNZA BUSTANI DARAJA LA II -  NAFASI 3 (LINARUDIWA)
9.1     MAJUKUMU YA KAZI
    Kupanda maua katika maeneo yanayohusika.
    Kupanda na kukata majani na kumwagilia maji.
    Kupanda mboga, matunda katika bustani.
    Kupalilia mazao katika bustani.
    Kufanya kazi zingine zitakazoelekezwa na Viongozi wa Kitengo chao.

9.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Cheti katika fani ya utunzaji bustani za maua, mboga na upandaji majani kutoka chuo cha Maendeleo ya Wananchi, VETA, au JKT au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali. 
9.3  MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGOS.A kwa mwezi.

10.0  AFISA WA SHERIA DARAJA LA II (LEGAL OFFICER GRADE II) – NAFASI 3(LINARUDIWA)
10.1  MAJUKUMU YA KAZI
Hili ni daraja la mafunzo katika kazi, hivyo Maafisa wa Sheria katika daraja hili watafanya kazi za kisheria kwa maelekezo ya Maafisa wa Sheria Waandamizi ikiwa ni pamoja na:
      Kutoa ushauri na kufanya utafiti wa kisheria pale anapohitajika kulingana na Wizara, Idara ya Serikali ama sehemu aliko.
      Kufanya mawasiliano na ofisi nyingine kuhusu masuala ya kisheria kwa maelekezo ya Maafisa wa Sheria walio katika ngazi za juu.

10.2 SIFA ZA MWOMBAJI 
Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza ya Sheria kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali na waliomaliza mafunzo ya uwakili yanayotambuliwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

10.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E Kwa mwezi

11.0  MSAIDIZI WA HESABU (ACCOUNTS ASSISTANT) - NAFASI
10(LINARUDIWA)
11.1  MAJUKUMU YA KAZI 
            Kuandika na kutunza “register” zinazohusu shughuli za uhasibu.  Kuandika hati za malipo na hati za mapokezi ya fedha.  Kutunza majalada yenye kumbukumbu za hesabu  Kupeleka barua/nyaraka za uhasibu Benki. 
            Kufanya usuluhisho wa masurufu, karadha, Hesabu za Benki na Amana.  


11.2  SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa wenye Cheti cha ATEC level II au “Foundation Level” kinachotolewa na NBAA  

11.3  MSHAHARA 
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.B kwa mwezi

12.0  MWENYEKITI WA MABARAZA YA ARDHI NA NYUMBA YA WILAYA
(CHAIRPERSON) – NAFASI 1.-INARUDIWA
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Makazi.
12.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kusikiliza, kuamua migogoro yote ya Ardhi na Nyumba kwa mujibu wa Sheria
Na 2 ya mwaka 2002 inayohu Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya Kusikiliza na kutoa uamuzi wa Rufaa kutoka Mabaraza ya Kata Kufanya marejeo kwa mashauri yaliyosikilizwa na mabaraza ya Kata.
      Kusimamia utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya na
      Mabaraza ya Kata katika eneo husika.

12.2 SIFA ZA MWOMBAJI
      Kuajiriwa wenye Shahada ya Sheria na kuendelea kutoka Chuo kikuukinachotambulika na serikali na kumaliza mafunzo ya kazini (internship)
      Awe na uzoefu wa miaka mitano (5) katika masuala ya Sheria na Kutoleauamuzi
      Awe mwadilifu na asiye na historia ya makosa ya jinai
      Awe na umri usiopungua miaka 35

12.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.J kwa mwezi.

13.0  FUNDI SANIFU MSAIDIZI (MAJI) (ASISTANT TECHNICIAN - WATER) NAFASI 2(LINARUDIWA)
13.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kupima uwingi wa maji mtoni
      Kusoma kituo cha hali ya hewa 
      Kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi. 

13.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha VI waliohudhuria na kufaulu mafunzo ya mwaka mmoja kutoka kutoka Chuo cha Maji au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali ambao wana cheti cha ufundi Daraja la  III katika fani ya maji.

13.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.

14.0  FUNDI SANIFU DARAJA LA II - UMEME (TECHNICIAN GRADE II ELECTRICAL) – NAFASI 4(LINARUDIWA)
14.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kufanya ukaguzi wa ubora wa magari ya Serikali na kurekebisha ipasavyo.
      Kufanya upimaji wa Mitambo na Umeme kufuatana na Maelekezo ya Mhandisi.
      Kufanya kazi za kutengeneza  magari,na vifaa vya Umeme
      Kufanya usanifu wa miradi midogo midogo ya umeme
      Kusimamia jinsi ya kufunga mashine mpya zinazowekwa kwenye karakana za ufundi na Umeme.

14.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye mojawapo ya sifa zilizotajwa hapa chini:
      Waliohitimu kidato cha VI na kufuzu mafunzo ya ufundi ya miaka miwili kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali katika fani ya ufundi Umeme.
      Waliohitimu kidato cha IV na kufuzu kozi ya ufundi ya miaka mitatu kutoka Vyuo vya Ufundi vinavyotambuliwa na Serikali  katika  fani ya ufundi Umeme,
      Wenye Cheti cha Majaribio ya Ufundi hatua ya I kutoka Chuo cha Ufundi kinachotambuliwa na Serikali,
      Wenye Stashahada ya Kawaida katika fani ya ufundi Umeme kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali.

14.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi


15.0  MCHAPA HATI DARAJA LA II – NAFASI 1(LINARUDIWA)
15.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kuchapa taarifa za Uthamini na Hati za fidia
      Kuchapa Nyaraka na Hati za kumiliki ardhi


15.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha Nne au cha Sita waliofaulu mtihani wa Uhazili Hatua ya II kutoka Chuo cha Watumishi wa Umma na ujuzi wa Kompyuta Hatua ya I na II kutoka Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
15.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS B 
16.0  KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III (PERSONAL SECRETARY GRADE III) – NAFASI 30(LINARUDIWA)
16.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida.
      Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
      Kusaidia kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa wakati unaohitajika.
      Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majadala, nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini.
      Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao.
      Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa Maofisa walio katika sehemu alipo, na kuyakusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika.
      Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na Msimamizi wake wa kazi.

16.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV waliohudhuria Mafunzo ya Uhazili na kufaulu mtihani wa Hatua ya Tatu.  Wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja na wawe wamepata mafunzo ya Kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti katika programu za Window, Microstoft Office, Internet, E-mail na Publisher.

16.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B kwa mwezi.

17.0  FUNDI SANIFU MAABARA MIFUGO DARAJA LA II (VETERINARY LABORATORY TECHNICIAN II) – NAFASI 5(LINARUDIWA)
17.1  MAJUKUMU YA KAZI 
      Kwa kushirikiana na Afisa Mifugo Msaidizi, atafanya uchunguzi wa magonjwa ya mifugo katika eneo lake. 
      Atakusanya sampuli kwa ajili ya uchunguzi wa maabara. 
      Kuwasaidia wataalam kuanda vifaa vya uchunguzi 
      Kutunza Usafi wa Maabara na vyombo vilivyomo. 
      Kutunza takwimu za uchunguzi  
      Atafanya kazi zingine zozote kama atavyopangiwa na mkubwa wake wa kazi  
17.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha sita (VI) waliofuzu mafunzo ya miaka miwili (2) ya Stashahada katika fani ya Fundi Sanifu Maabara (Mifugo) kutoka Chuo cha Mifugo (LITI), au chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali. 

17.3 MSHAHARA  
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGS C kwa mwezi

18.0  MSAIDIZI USTAWI WA JAMII II (SOCIAL WELFARE ASSISTANT) – NAFASI  2 (LINARUDIWA)
18.1  MAJUKUMU YA KAZI 
      Kutambua na kuhudumia watu walio katika makundi maalum na mazingira hatarishi 
      Kukusanya takwimu zinazohusu watu walio katika makundi maalum na mazingira hatarishi 
      Kuchambua na kuandaa orodha ya maombi mbalimbali kutoka kwenye familia na watu wenye dhiki 
      Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake

18.2 SIFA ZA MWOMBAJI  
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne au sita na wenye cheti cha mafunzo ya mwaka mmoja ya Ustawi wa Jamii kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali. 

18.3 MSHAHARA  
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS C Kwa mwezi.
     
19.0 MTHAMINI DARAJA LA II (VALUER GRADE II) – NAFASI 7(LINARUDIWA) 19.1 MAJUKUMU YA KAZI
      Kukusanya taarifa za utafiti na mwenendo wa soko la ardhi.
      Kuhakiki kumbukumbu za utafiti na kuziingiza kwenye kompyuta

19.2 SIFA ZA MWOMBAJI
      Kuajiriwa wenye Shahada/Stashahada ya juu katika fani ya Usimamizi Ardhi na
Uthamini (Land management and Valuation) kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi au Taasisi nyingine zinazotambuliwa na Serikali katika fani za Usimamizi Ardhi na Uthamini. Au
      Kuajiriwa wenye cheti cha NCPS katika fani ya Usimamizi Ardhi na Uthamini.

19.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali TGS E kwa mwezi.

20.0  FUNDI SANIFU DARAJA II - UPIMAJI  NAFASI 3(LINARUDIWA)
20.1  MAJUKUMU YA KAZI
Sehemu ya Topographic and Geodetic Survey:
Kupanga na kuandaa mahitaji ya kambi za upimaji, vifaa vya upimaji na mahitaji ya jumla.

20.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Diploma ya kawaida katika fani ya Upimaji Ardhi, kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali na wenye uzoefu wa kazi kwa muda usiopungua miaka mitano.

20.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi

21.0  MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II–HOME ECONOMICS/ DOMESTIC SCIENCE   
(NAFASI 4)(LINARUDIWA)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la ushonaji, ufumaji, kudarizi, upishi na lishe katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara

21.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kufundisha masomo ya ushonaji, ufumaji, kudarizi na upishi na lishe katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
      Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
      Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
      Kutunza vifaa vya kufundishia
      Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
      Kutoa  Ushauri wa kitaalam
      Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
      Kutunga na kusahihisha Mitihani
      Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
      Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
21.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya ufundi katika fani zaushonaji, ufumaji, kudarizi, upishi na lishekutoka vyuo vya ufundi vinanvyotambuliwa na Serikali. 

21.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS Ckwa mwezi.

22.0  MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II- ELECTRICAL ENGINEER - (NAFASI 10) (LINARUDIWA)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Umeme wa majumbani (Electrical installation), computer application na technical drawing katika vyuo vya maendeleo ya Jamii Tanzania Bara
22.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kufundisha somo la umeme wa majumbani, computer application na technical drawing katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
      Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
      Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
      Kutunza vifaa vya kufundishia
      Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
      Kutoa  Ushauri wa kitaalam
      Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
      Kutunga na kusahihisha Mitihani
      Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbaimbali katika jamii inayoizunguka chuo
      Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo

22.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Mafunzo ya stashahada katika fani ya Umeme kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.  

22.3  MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.

23.0  MKUFUNZI DARAJA LA II- MHANDISI UJENZI (CIVIL ENGINEER)-(NAFASI 4)(LINARUDIWA)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wahandisi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Ujenzi katika vyuo (24) vya maendeleo ya Wananchi na chuo cha Maendeleo ya Jamii Missungwi

23.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kufundisha somo la uungaji vyuo, computer application na Technical drawing katika vyuo vyuo vya maendeleo ya wananchi.
      Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
      Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
      Kutunza vifaa vya kufundishia
      Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
      Kutoa  Ushauri wa kitaalam
      Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
      Kutunga na kusahihisha Mitihani
      Kufanya Utafiti utakaosaidia kutoa majibu kwa matatizo/changamoto mbaimbali katika jamii inayoizunguka chuo
      Kutoa ushauri juu ya kuboresha taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo

23.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika fani ya Uhandisi Majengo(Civil Engeneering) kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali

23.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS Dkwa mwezi.

24.0      MPOKEZI (RECEPTIONIST) – NAFASI 1 (LINARUDIWA)
24.1      MAJUKUMU YA KAZI
      Kupokea wageni na kuwasaili shida zao.
      Kutunza rejesta ya wageni wa ofisi na kufanya uchambuzi wa wageni wanaoingia ili kutoa ushauri juu ya utaratibu bora wa kupokea wageni.


Kupokea na kusambaza maombi ya simu za ndani.
      Kutunza na kudumisha usafi wa “Switchboard” na ofisi zake.
      Kuwaelekeza wageni wa ofisi kwa maafisa/ofisi watakakopewa huduma.
      Kuhakikisha kwamba wageni wanaoingia ndani wanamiadi (Appointment) au wamepata idhini ya maafisa husika.
      Kupokea simu kutoka nje na kuzisambaza kwa maofisa mbalimbali ofisini.
      Kupokea simu kutoka “Extension” za ndani na kupiga nje ya ofisi.
      Kutunza rejesta ya simu zinazopokelewa kutoka nje ya ofisi na zinazopigwa kwenda nje.

24.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha IV waliofaulu masomo ya Kiingereza, Kiswahili na Hisabati na kufuzu mafunzo ya Mapokezi na Upokeaji Simu kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

24.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B kwa mwezi

25.0      MHANDISI II  UFUNDI (MECHANICAL ENGINEER) – NAFASI 20
25.1      MAJUKUMU YA KAZI
    Kufanya kazi chini ya uangalizi wa Mhandisi aliyesajiliwa na bodi ya usajili wa Wahandisi kama Professional Engineer ili kupata uzofu unaotakiwa.
    Kufanya kazi kwa vitendo katika fani ya Mekanika ili kumwezesha kupata sifa za kutosha kusajiliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi.
    Kukusanya taarifa na takwimu kuhusu magari na mitambo mbalimbali, bei za magari na mitambo na vifaa vya umeme ndani na nje ya nchi.
    Kupitia mapendekezo ya miradi (project proposals) mbalimbali ya Ufundi .

25.2 SIFA ZA MWOMBAJI
    Kuajiriwawenye Shahada/Stashahada ya juu ya Uhandisi (Mechanical Engineering) kutoka vyuo vikuu vinavyotambulika na Serikali. 

25.3 MSHAHARA
    Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS Ekwa mwezi.

26.0 FUNDI SANIFU DARAJA LA II - MITAMBO (TECHNICIAN GRADE II

MECHANICAL) – NAFASI 4(LINARUDIWA)
26.1 MAJUKUMU YA KAZI
      Kufanya ukaguzi wa ubora wa magari ya Serikali na kurekebisha ipasavyo.
      Kufanya upimaji wa Mitambo kufuatana na Maelekezo ya Mhandisi.
Kufanya kazi za kutengeneza  mitambo na magari
      Kufanya usanifu wa miradi midogo midogo ya mitambo
      Kusimamia jinsi ya kufunga mashine mpya zinazowekwa kwenye karakana za ufundi .

26.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye mojawapo ya sifa zilizotajwa hapa chini:
      Waliohitimu kidato cha VI na kufuzu mafunzo ya ufundi ya miaka miwili kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali katika fani ya ufundi Mitambo.
      Waliohitimu kidato cha IV na kufuzu kozi ya ufundi ya miaka mitatu kutoka Vyuo vya Ufundi vinavyotambuliwa na Serikali  katika  fani ya ufundi Mitambo,
      Wenye Cheti cha Majaribio ya Ufundi hatua ya I kutoka Chuo cha Ufundi kinachotambuliwa na Serikali,
      Wenye Stashahada ya Kawaida katika fani ya ufundi Mitambo kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali.

26.3 MSHAHARA
      Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi

27.0  AFISA ELIMU DARAJA LA II –NAFASI 1

27.1  MAJUKUMU YA KAZI
      Kufundisha katika Chuo cha Madini Dodoma kufuatana na masomo aliyosomea.
      Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia/kujifunzia,mazoezi ya wanafunzi na wanachuo.
      Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanafunzi na wanachuo.
      Kuandaa,kuwapangia kazi wanafunzi/wanachuo na kusahihisha mazoezi
      Kuandaa taarifa kuhusu kazi za wanafunzi/wanachuo nakuwasilishwa kwa uongozi wa shule/chuo.
      Kuandaa na kutunza kumbukumbu za wanafunzi/wanachuo na kuwasilishwa katika mamlaka husika.
      Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu
      Kusimamia vyama vya masomo(Association).
      Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa shule/chuo
      Kusimamia”clubs” za masomo
      Kuandaa mpango kazi na kutoa kipaumbele kwa majukumu kulingana na upatikanaji wa nyenzo.
      Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa Kufanya shughuli za ukuzaji mitaala
Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Kituo

27.2 SIFA ZA MWOMBAJI 
      Kuajiriwa wenye Shahada ya Elimu katika fani ya Hesabu na Sayansi ya Kompyuta(Computer Science) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es  salaam au vyuo vingine vingine vinavyotambuliwa na Serikali

27.3 MSHAHARA
      Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS.D kwa mwezi



                                             X.M. DAUDI
                                                 Katibu
               Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.